Hata kama mtoto haumwi na tumbo , kumnyamazisha motto anayelia ni vigumu sana . Kama umejaribu kila mbinu na hujafaulu , jaribu yafuatayo:
- Mfunge mtoto kwenye vitambaa au blanketi ili ahisi joto kiasi na atulie.
- Jaribu kucheza muziki muororo au muimbie nyimbo za kumbembeleza.
- Mbebe kwa makini au nenda matembezi naye katika gari lako na hakikisha umemkalisha nyuma.
- Kumkanda mgongoni au tumboni kwa weza kumliwaza hasa kama ana hewa tumboni.
- Kumnyonyesha kwa weza kutuliza mdundo wa roho yake kutuliza tumbo lake na viungo pia.
Habari njema ni kuwa watoto hupita hatua hii wanapokuwa. Mtoto wako anapokuwa wiki 6 au 8 watakuwa katika hali ya kuweza kujiliwaza na kulia kwingi kutakwisha.